Monday, October 12, 2015

MAHAKAMA YAAGIZA WATOTO WA MUBARAK WAACHILIWE!

Wanawe Mubarak
Mahakama nchini Misri imeagiza kuachiliwa huru wa wana wawili wa kiume wa rais aliyeng’olewa mamlakani Hosni Mubarak.
Wawili hao walikuwa wamefungwa jela miaka mitatu kwa kuhusika katika ufisadi, shirika la habari linalomilikiwa na serikali Nile News limeripoti.
Mahakama iliamuru Alaa na Gamal Mubarak waachiliwe huru baada ya kuzingatia muda ambao wamekaa jela, afisa wa mahakama na wakili wao Farid al-Deeb wameambia shirika la habari la AFP.
Wawili hao walikamatwa na kuzuiliwa mwaka 2011.
Bado wanasubiri uamuzi kuhusu rufani waliyokata dhidi ya hukumu nyingine ya miaka mitatu jela kila mmoja kwa ubadhirifu wa pesa za umma.
Walikuwa pia wanatajwa katika kesi kuhusu kuingilia na kuchezea soko la hisa.
Chanzo:-BbcSwahili

Tags:
Unknown About Unknown

Hii ni blog kwaajili ya kukupa habari za kila aina ulimwenguni ili usiweze kupitwa na jambo habari mpya,michezo,burudani,sanaa,nyimbo mpya,video@Nuru fm Newsroom/production
View all posts by admin →

Get Updates

Subscribe to our e-mail newsletter to receive updates.

Share This Post

0 comments:

Facebook Blogger Plugin: Bloggerized by Nuru fm Iringa Enhanced by Joseph Martin

© 2015 NURU FM. NURU FM JOSEPH Y. converted by NURU FM NEWSROOM
Powered by Blogger.