Mahakama ya Mwanzo ya Dodoma Mjini akishtakiwa kwa matumizi mabaya ya
mtandao.
Sospiter alisomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Mussa
mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo Emmanuel Bwile.
Mshtakiwa huyo anadaiwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook ujumbe
kuwa “Pinda utakuwa muhubiri wa injili tu.”
Mussa aliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa huyo alibandika picha ya John
Maliga kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika ujumbe huo, kitendo
ambacho ni kinyume cha kifungu namba 16 cha Sheria ya Mtandao ya Mwaka 2015.
Mlalamikaji katika shauri hilo la jinai namba 815/2015 litakalokuja tena
mahakamani Oktoba 19, ni John Maliga.
Mshtakiwa yupo nje baada ya kutimiza masharti ya dhamana iliyomtaka kuwa
na mdhamini mmoja na bondi ya Sh1 milioni.
Kesi hii imekuja baada ya wiki iliyopita, kijana mmoja, Benedict
Ngonyani (24) kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es
Salaam akituhumiwa kusambaza taarifa za uongo zinazomhusu Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Davis Mwamunyange.
Kijana huyo anatuhumiwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook na
WhatsApp kuwa, Mwamunyange, amelazwa kwenye hospitali moja mjini
Nairobi, Kenya kwa madai ya kulishwa chakula chenye sumu.
Unknown
No comments: